ONYESHO LA MALKIA
Kwa walio wengi siku ya muhimu sana katika maisha ni siku ya ndoa au siku ya Harusi, ni siku inayokutanisha nyoyo mbili tofauti za watu wawili tofauti kwa pamoja na familia zao kwa sababu ya kusherehekea na kula mapochopocho ambayo roho inapenda baada ya miezi isiyopungua sita ya maandalizi mazito ili kuhitimisha harusi rasmi.
Harusi siyo harusi bila mavazi ya aina yake hivyo Mustafa hasanali mbunifu maarufu wa mavazi hapa nchini atafanya onyesho la mavazi ya harusi tarehe 7/2/2009 pale little Theatre Club karibu na ST. Peter Oysterbay, mustafa ni ameshabuni mavazi tofauti ya harusi mbalimbali na hivi sasa anakuja na kitu cha kipekee kwa Bi. harusi mtarajiwa ili kumuandaa kuhitimisha siku hii ya muhimu kabisa.
Pamoja na misukosuko ya kibiashara duniani maisha lazima yasonge mbele na hasa katika dunia yetu maridhawa ambapo ili mteja aweze kupata kitu kizuri zaidi lazima agharimie hivyo Zain, Stella Artois na MOTOMEDIA watafanikisha onyesho la Malikia kwa udhamini wao mzuri kwetu waandaaji wa onyesho la Malkia.
Iwe ni Ktchen Party Send Off au harusi yenyewe bila shaka mwanamke wa kisasa atapatachaguo la mavazi ya harusiya kipekee kutoka hapahap nyumbani kwa kuwa hakuna kisichowezekana - pamoja tunaweza
0 comments:
Post a Comment