
Ziara hii ya warembo ni ya kimafunzo kabla hawajapanda jukwaani julai 2 kwa lengo la kujifunza mambo mbalimbali yanayofanywa katika utayarishaji wa gazeti hilo.
Warembo hao wanatarajiwa kuchuana katika kinyang'anyiro kitakachofanyika ijumaa wakiwania taji hilo kwenye ukumbi wa Mlimani City uliopo Chuo Kikuu cha Mlimani jijini Dar es salaam, katika shindano hilo burudani itatolewa na vijana machachari kutoka kundi la THT la jijini Dar es salaam pamoja na Sebene la kukata na shoka kutoka kwa vijana wa African Stars wana wa (Kutwanga na kupepeta).
0 comments:
Post a Comment