Katika mchezo wa leo taifa Stars ilizidiwa sana katika kiungo kwenye kipindi chote cha kwanza lakini mabadiliko yaliyofanyika kipindi cha pili kwa kumtoa Kigi Makasy na kumwingiza Mussa Hassan Mgosi yalizaa matunda kwa kuleta nguvu mpya iliyosababisha mshambuliaji Mrisho Ngasa kusawazisha goli baada ya Taifa Stars kufungwa dakika za mwanzo tu na mchezaji Roger Thous wa Rwanda.
Matokeo haya yanaipa wakati mgumu timu ya Taifa Stars wakati watakapokwenda Nchini Rwanda kurudiana na Amavubi katika jiji la Kigali, kwani inabidi washinde tu ili kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kusonga mbele katika michuano hii ya komba la mataifa huru ya Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN kwani suluhu ya aina yoyote haitaisaidia chochote Taifa Stars.
0 comments:
Post a Comment