![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhbvHOybr6N0QfP56UbkNtgptSrzCWq-F3exT0D4X6cJvsX0IVjxk61aAIgkUp5mpU0PeSbhO4Y60BFvHCCgayfe1dww9ebbAtCfVRSkPGtnwl-axhQZNKcKi7xTx73IGkMaY6yiVL8lpNP/s400/602.jpg)
Simba ambayo itaongozwa na Kocha wa timu hiyo mzambia Patrick Phiri na mwenye mafanikio makubwa katika timu hiyo ya Mtaa wa Msimbazi inawahi kwenda huko ili kuzoea hali ya hewa na kusoma mazingira ya Misri kabla ya mchezo wao huo ambapo katika mchezo wa awali kwenye uwanja wa Taifa Simba iliwafunga waarabu hao magoli 2 kwa 1 wiki iliyopita.
Ili kuendelea katika michuano hiyo Simba inahitaji ushindi wa aina yoyote au suluhu ili iweze kuwakilisha vyema Tanzania katika mashindano hayo, hata hivyo timu hiyo ina rekodi nzuri dhidi ya timu za misri na imekuwa ikifanya vyema mara kadhaa inapokutana na timu hizo mfano mzuri ni pale ilipoivurumusha katika michuano timu ngumu ya Zamalek ambayo ilikuwa ni bingwa mtetezi wa Klabu bingwa Afrika mwaka 2003.
0 comments:
Post a Comment