
Amesema katika mapambano hayo mikoa saba itakutanisha wapiganaji wake ili kupata washindi watakaoingia kwenye nusu fainali na kisha fainali zinazotarajiwa kufanyika machi 6 /2010 huku zikikutanisha pia wapiganaji wanawake Upendo Njau kutoka Tanzania na Sarah Scott kutoka Afrika Kusini.
Mikoa inayotarajiwa kushiriki katika ligi hiyo na mabondia ni Chande Ali (Lindi), Charles Hangaya (Mwanza), Emmanuel Shija(Shinyanga), Master Shemboko( Muheza), Kanda Kabongo( Dar es salaam) Maiko Deus( Mara), Mrisho Shabaan(Musoma), Putile Gama(Ruvuma) na Khamis Mwakinyo( Tanga)
Zawadi ya mshindi wa kwanza katika ligi hiyo ni Pikipiki kubwa yenye thamani ya shilingi milioni 6 na mipango inafanywa ili kuboresha zawadi kwa washindi wengine wa pili na wa tatu hivyo Japhetn Kaseba ambaye ni mwandaaji ametumia nafasi hiyo kuwaomba watu na makampuni mbalimbali wenye mapenzi mema na mchezo huo, kujitolea na kudhamini ligi hiyo ili kuwapa moyo wachezaji wetu ambao pia inatarajiwa kuwa timu ya taifa ya mchezo huo itatoka katika michezo hiyo.
0 comments:
Post a Comment