Amesema mwisho wa kupeleka maombi hayo itakuwa februari 28 2010 na baada ya hapo tume hiyo itapitia maombi hayo na kuona ni mikoa na wilaya gani zimekidhi na kufuata maelekezo ya tume hiyo ili majimbo yao yaweze kugawanywa, gharama halisi itakayotumika ktika shughuli za kugawa majimbo ni shilingiMilioni 50.
Akizungumzia gharama za uchaguzi wa mwaka huu Mwenyekiti wa tume hiyo Rajabu Kiravu amesema gharama hizo zimegawanyika katika awamu tatu ambapo uboreshaji wa Dafrtari la wapiga kura awamu ya kwanza uligharimu shilingi Bilioni 27 na awamu ya pili uligharimu shilingi bilioni 42 na uchaguzi mkuu utagharimu shilingi bilioni 64.
Tanzania inatarajiwa kufanya uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani hapo baadae mwaka huu na vyama mbalimbali viko katika pilikapilika za kujiandaa na uchaguzi huo baada ya awamu ya kwanza ya kipindi cha miaka mitano ya Rais Jakaya Kikwete kumalizika, aliye kulia katika picha ni mwenyekiti wa tume ya uchaguzi (NEC) Rajabu Kiravu.
0 comments:
Post a Comment