Yogayoga alizaliwa mwaka 1978 Wilayani Mpanda katika mkoa wa Rukwa na alianza shule ya msingi mkoani humo mwaka 1987 na baadae mwaka 1989 alihamia mkoani Dodoma ambapo alisoma shule ya msingi ya Majengo na kumalizia elimu ya msingi shuleni hapo baadae alijiunga na shule ya Sekondari Mazengo alisoma hapo kuanzia kidato cha kwanza mpaka cha tatu, lakini alishindwa kuendelea na masomo na kujiunga na vikundi vya mchezo wa Sarakasi, aliendlea na michezo hiyo na kufanya kazi na wasanii tofauti kama vile Saida Karoli na Wanne Star ilipofika mwaka 2007 aliondoka kwenda nchini Ujerumani kwa ajili ya maonyesho ya Sarakasi na kujiendeleza zaidi kimasomo ambapo kwa sasa ameungana na wasanii mbalimbali wa nchi za kiafrika na wamekuwa wakifanya maonyesho katika nchi tofauti za Ulaya na Marekani huku akiendelea na masomo ya kutengeneza vipindi na uongoza ji wa Filamu FULLSHANGWE inampa Bravo Yogayoga kwa juhudi zake hizo na inamtakia mafanikio mema kwa picha zaidi shuka chini mdau.
MWANASARAKASI YOGAYOGA ATAMBA NCHINI UJERUMANI!!
Posted by
ADMIN
You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment