Ilikuwa ni miaka ya mwishoni mwa tisini ambapo kundi la Love Forever lililokuwa linajumuisha wasanii Mr Simple na Marine Man lilikuwa juu sana baada ya nyimbo zao kama 'Umbo' na 'Shory' kuwa gumzo na kupigwa sana kwenye vituo mbalimbali vya televisheni na redio nchini.
Baadaye waliachia albam ambayo kwa hakika haikuweza kuuza mpaka kufikia malengo yao hivyo wakaamaua kukaa benchi huku wakiusoma mchezo unavyokwenda.
Mwaka 2005,Renatus Pamba au kama anavyojulikana kama Mr Simple aliamua kutoka yeye kama yeye na kuona ya kwamba anaweza akafanya kitu na watanzania kupendenzwa nacho.Ndipo alipoachia wimbo wake mwenyewe akiwa kama mwanamuziki wa kujitegeemea uliokuwa unaitwa 'Mr Simple' aliomshirikisha mwanadada Jackline.
Wimbo huo uliokuwa kwenye mahadhi ya dancehall nao uliweza kupigwa kwenye vituo mbalimbali vya redio nchini.
Mwaka uliofuata,Simple aliachia nyimbo nyingine mbili kwa mpigo,'Father Of Dancehall' na 'kamata chati mbambali.
Tokea kipindi hiko chote,Mr Simple aliamua kupumzika kuhusu masuala ya muziki na kuamua kujishughulisha na shughuli nyingine.
“Niliamua kupumzika masuala ya muziki kidogo ili niweza kufanya shughuli zangu nyingine ambazo nilikuwa nahitaji muda mwingi kuzitekeleza na ndiyo maana sikuweza kusikika kwa takribani miaka mitatu.”Simple
Mwaka huu Mr Simple amedhamiria kufnaya mapinduzi halisi kwenye muziki wa dancehall nchini na mashabiki wake.
Mwanamuziki huyu aliongea na starehe na kusema ya kwmaba anarudi kwa nguvu zote mpaka aone ya kwmaba muziki wa aina ya dancehall unakubalika kama aina nyingine ya muziki hapa nchini.
“Nimerudi na sasa kwa nguvu zote,nawahakikishia ya kwamba nitafanya mapinduzi halisi,nataka kuutangaza vyema muziki wa dancehall nchini,sio kila siku tunang’ang’ania aina moja ya muziki,dancehall ni muziki bora ambao unahitaji kukubalika”Alisema.
Alipoulizwa ya kwamba kwa nini anasema ya kwamba dancehall ni muziki bora kuliko aina nyingine ya muziki,Simple alijibu ya kwmaba muziki huo ni bora kwasababu unachezeka na vilevile haupitwi na wakati kamwe.
“Sijawahi kusikia dancehall umepitwa na wakati,leo ukiwekewa nyimbo ya Sean Paul ya kwanza kabisa utasimama na kucheza,na ndiyo maana naamini ya kwamba dancehall ni muziki bora zaidi kulikko aina nyingine ya muziki .
“Ukifanikiwa kusikiliza nyimbo zangu mpya,utaamini haya nayosema kwakuwa kuna ladha flani ambazo lazima zitakuamsha kutoka kwenye kiti chako na kuanza kucheza,nyimbo zangu zote zinachezeka na sisiti kujisifia hilo kabisa kwakuwa naamini kile kitu ambacho nachokifanya”Alisema.
Albam ya Mr Simple itakayoijulikana kwa jina la ‘Father Of Dancehall’ ambayo anatarajia kuiachia mapema mwakani inatarajia kuwa na vibao nane vikiwemo vingine kama ‘Naapa’,’Senorita’ pamoja na ‘Nimestuka’ wimbo ambao ndio ataanza kuuachia kwanza.
Aliweza kufafanua kwanini ameamua kuiita albam yake hiyo ‘Father Of Dancehall’ kwamba anaamini yeye ndiye mkubwa wa muziki huo wa dancehall nchini na ndiyo maana ameamua kuiita albam yake jina hilo.
“Mimi ndiye ‘Father Of Dancehall’ hakuna ubishi kuhusu hilo hapa nchini,na hiyo ndiyo sababu kubwa iliyosababisha niite albam yangu jina hilo”Simple.
Mbali na hayo yote,Simple alisema ya kwamba kamwe hawezi kufanya aina yeyote ya muziki zaidi ya dancehll kwakuwa ndio muziki ambao upo kwenye hisia zake saa zote hivyo hajawahi kuimba muziki wowote tofuati na dancehall na hatowahi kujaaribu kufanya hivyo.
Kabla ya kuwa mwanamuziki,Mr Simple alianza kwa kuwa Disko Joka,au kwa kifupi DJ huko mkoani Shinyanga na baadaye kuamaua kuacha kazi hiyo na kujikita kwenye muziki huku akiungana na mwezake kwa pamoja wakaunda Love Forever ambalo liliweza kudumu kwa takribani miaka sita na baadaye kuvunjika mwaka 2005.
Simple alipenda kuwashauri wanamuziki nchini kutokata tamaa labda baada ya kuona nyimbo zao hazipigwi kwenye redio,kwani alisema kila kitu kina muda wake muafaka hivyon watulize vichwa na kuanza upya.
“Wale wote waliojaribu kuimba na kukata tama,nawashauri watulize vichwa na kuangalia uystaarabu mwingine wa kutoka,nasema hivi kwasababu nina maana yangu,muziki hauhitaji pupa,wengie wameingia kwa pupa sasa hivi hawasikiki tena”Alisema.
Shukrani zake kwa dhati zinamuendea Mwenyezi Mungu kwani anaamini ya kwamba Mwenyezi Mungu ndiye aliyemfikisha hapo alipo leo,hivyo kama asipomshukuru atakuwa hatendi haki na vilevile mashabiki wake wote.
Mwanamuziki huyo alisema ya kwmaba Tanzania imejaliwakuwa na wanamuziki wenye vipaji hivyo wanatakiwa kufanyia kazi vipaji hivyo ili waweze kusikika kimataifa.Aliweza kumtolea mfano mwanamuziki Banana kwa kusema ya kwamba Banana nimwanamuziki mzuri lakini anahitaji kusikika zaidi nje ya Tanzania ili aweze kukubalika.
“Nimeweza kushuhudia wanamuziki mbalimbali kwa muda niliokaa nao,nimependa jinsi Banana anavyofanya kazi zake,kwani ni mwanamuziki aliyebarikiwa kuwa na kipaji.Mbali na hayo, De Plaizir atarekodi nyimbo moja na mwanamuziki huyo pamoja na baadhi ya wanamuziki kutoka bendi ya Akudo kwakuwa anahitaji kupata kumbukumbu ya wanamuziki kutoka nchini.
“Narekodi ngoma na Banana pamoja na baadhi ya wanamuziki wa Akudo ili tu niweze kuweka kumbukumbu yangu hapa nchini,wimbo utakuwa bora na wakimataifa zaidi,kaeni tayari”Alisema.Mwanamuziki huyo ambaye anatarajia kuondoka nchini wiki hii baada ya kukamilisha kazi ya kurekodi na wanamuziki hao.
0
comments
Saturday, September 27, 2008
0
comments
Friday, September 26, 2008
Msemaji mkuu wa kampuni ya Cellulnt Bw. Khamis Dacota akielezea jambo kwa wageni waalikwa katika uzinduzi wa kampuni hiyo itakayojihusisha na uuzaji wa milio ya simu za mkononi kwa kutumia nyimbo za wasanii wa hapa nchini kampuni hiyo ipo katika nchi kadhaa za Afrika kama Nigeria, Ghana, Kenya Uganda na sasa Tanzania uzinduzi huo ulifanyika kwenye Hotel ya Southern Sun Jijini Jana 25/09/2008
0
comments
Thursday, September 25, 2008
0
comments
Wednesday, September 24, 2008
0
comments
Monday, September 22, 2008
0
comments
Saturday, September 20, 2008
0
comments
Wednesday, September 17, 2008
Wageni mbalimbali walijitokeza kwenye Tamasha la muziki na chakula cha utamaduni wa Norway lililotumbuizwa na kundi la Umoja Cultural Flying Carpet linalounganisha wasanii kutoka Tanzania Mosambique na Norwy tamasha hilo lililoandaliwa na ubarozi wa Norway nchini katika Hotel ya Movenpick mwanzoni mwa wiki
Mji wa Tabora unavyoonekana kwa chini Picha hii ametutumia mdau Gerald Hando aliyekuwepo kwenye Safari hiyo ya kwanza, mara baada ya ATC kuanzisha Rout ya Dar, Tabora na Kigoma.
0
comments
Tuesday, September 16, 2008
Mwenyekiti wa Yanga Imani Mahugila Madegaa linaswa na Camera ya FULLSHANGWE akipunga upepo katika viwanja vya Readers mara baada ya timu yake kupata ushindi dhidi ya mtibwa kushoto ni mkurugenzi wa simba Evarist Hagila Na kulia ni Shabiki mkubwa wa Yanga Phill Mmari.
0
comments
Monday, September 15, 2008
0
comments
Sunday, September 14, 2008