Naibu Waziri wa habari Michezo na Utamaduni Joel Bendera akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa Ligi Kuu yaVodacom iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam leo mara baada ya ligi hiyo kumalizika hivi karibuni na simba kuibuka kidedea kwa ktofungwa hata mchezo mmoja hivyo kuukwaa ubingwa huo kwa historia ya kipekee.
Waziri Bendera ameipongeza Simba kwa kuchukua ubingwa kwa staili ya aina yake lakini pia akapongeza vilabu vingine kwa kufanya vizuri katika ligi hiyo, ameongeza kwa kusema utawala bora na kufuata kanuni za mchezo wa soka ni kitu muhimu sana na si vizuri watu wa mpira kwenda mahakamani kutafuta kile wanachokiita kahi wakati kanuni zipo wanaweza kuzifuata na kupata haki zao.
Simba mbali ya kuwa mabingwa wa ligi ya Vodacom 2009-2010 imefanikiwa kutoa Kocha bora wa ligi, mfungaji bora na Kipa bora huku mchezaji aliyesaidia kwa uwezo wake wote timu yake akiwa Mrisho Ngassa wa Yanga.
Yanga imechukua milioni 15 huku timu ya Azam FC ikichukua zawadi yake ya milioni 10 na timu ya Africa Lion ikachukua shilingi milioni 5 kwa kuwa timu yenye nidhamu katika Ligi kuu ya Vodacom.
Katibu Mkuu wa shirikisho la soka nchini TFF akizungumza mbele ya wageni waalikwa waliojitokeza kushuhudia hafla ya kukabidhi zawadi za washindi wa ligi kuu





0 comments:
Post a Comment